Uchambuzi wa tamathali za usemi pamoja na mbinu nyingine za matumizi ya lugha katika utenzi wa mikidadi na mayasa
Abstract
Utafiti huu unahusu uchambuzi wa tamathali za usemi na mbinu nyengine za matumizi ya lugha katika Utenzi wa Mikidadi na Mayasa na Said Abdalla Masudi
el Buhry el Hinawy. Kazi hii imegawanywa katika sura nne, Katika sura ya kwanza tumeelezea swala letu la utafiti, madhumuni ya utafiti na nadharia tete zinazotuongoza. Isitoshe tumeeleza sababu za kuchagua mada hii pamoja na kufafanua upeo na mipaka ya somo hili, yaani utafiti wetu. Pia tumefafanua msingi wa kinadharia wa utafiti pamoja na yaliyoandikwa kuhusu somo hili, mbinu za utafiti na uchanganuzi wa data. Katika sura ya pili tulitanguliza kwa kueleza maana ya fani pamoja na kuvitolea maelezo vipengele mbalimbali vya fani kikiwemo kipengele cha tamathali za usemi na mbinu nyingine za matumizi ya lugha.Tumewarejelea wataalamu mbalimbali katika kurejelea vipengele hivyo. Sura ya tatu tumebainisha tamathali tofauti tofauti za usemi pamoja nambinu nyingine za matumizi ya lugha zilizotumika katika utenzi huu na kuzitolea maelezo yake. Sura ya nne ni hitimisho.Tumeeleza tuliyoyatambua na kutoa mapendekezo ya utafiti zaidi.
Publisher
University of Nairobi, Kenya