Umaanisho Katika Tamthilia Ya Mama Ee Ya Mwachofi
Abstract
Mchakato mzima wa kuikamilisha tasnifu hii haukuwa kwa bidii zangu mwenyewe bali iliweza kufanikishwa kutokana na michango na msaada wa wengine. Kwanza kabisa ninamtolea Mwenyezi Mungu kwa fadhili zake na kunipa nguvu za kukabiliana na changamoto mbalimbali wakati nikiitafitia mada hii. Mwenyezi Mungu pia aliweza kunipa hamu ya kuendelea na kutokata tamaa wakati wa kufanya utafiti huu hasa pale nilihisi kulemewa na changamoto za maisha. Kwa hivyo sina budi kumtukuza na kumheshimu kila wakati. Pili natoa shukrani zangu kwa wasimamizi wangu Prof. Habwe na Bi. Mary Ndung‟u kwa kuniongoza na kunielekeza katika kuiandaa kazi hii kuanzia mwanzo hadi mwisho. Kwa hakika mmeniongoza na kunifanya kujifunza mengi kuhusu utafiti huu. Msingenielekeza, kwa kweli ingekuwa vigumu kufanya utafiti huu. Asanteni sana kwa uvimilivu wenu kwangu katika kunikosoa na kunielekeza hadi nikafika kiwango hiki. Shukrani sana na Mungu awabariki.Vilevile, ningependa kutoa shukrani zangu kwa wahadhiri wote wa Chuo Kikuu cha Nairobi, idara ya Kiswahili. Mafunzo na ushauri wenu ndio ulionipa motisha na hamu ya kuifanya kazi hii na kuikamilisha, nawashukuru nyote na Mwenyezi Mungu awabariki kwa kazi nzuri mnayoifanya.Mwisho, ningependa kuwashukuru rafiki zangu wa dhati ambao wameweza kupitia mkondo huu kwa ushauri wao kwangu. Waliniongoza na kunishauri hadi mahali hapa nimefika. Nao ni pamoja na Pamela Alekana, Braicy Inziani na Gladys Kinyua. Hakika mmekuwa rafiki zangu wa karibu mmefaa kila wakati nilipohitaji usaidizi wenu. Mungu awabariki na muendelee na moyo uo huo.
Publisher
University of Nairobi
Subject
Tamthilia Ya Mama Ee Ya MwachofiRights
Attribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United StatesUsage Rights
http://creativecommons.org/licenses/by-nc-nd/3.0/us/Collections
The following license files are associated with this item: