dc.description.abstract | Tasnifu hii inahusu jumbe zinazopatikana katika magari ya usafiri wa umma yanayojulikana
kama Matatu. Utafiti wetu umefanyiwa mjini Nyahururu ambao ni mji unaopatikana katika
jimbo la Nyandarua, takribani kilomita mia moja themanini kaskazini mwa jiji kuu la Kenya,
Nairobi.
Utafiti huu umegawanywa katika sura tano. Katika sura ya kwanza, tumelenga kutanguliza
mada, tatizo la utafiti, madhumuni ya utafiti na nadharia tete zitakazotuongoza katika utafiti
wetu.
Aidha tumeziangalia sababu zetu za kuchagua mada pamoja na upeo na mipaka ya uchunguzi
wetu, yaliyoandikwa kuhusu mada yetu, msingi wa nadharia na hatimaye mbinu zilizotumika
katika utafiti huu.
Sura ya pili imelenga kuchunguza mitindo iliyotumiwa katika maandishi ya vibandiko. Sura ya
tatu imeshughulikia matumizi ya sentensi na tamathali za userni pamwe na jumbe katika
matatu.
Katika sura ya nne, tumechunguza hisia na maoni ya wasafiri na waandishi wa jumbe zenyewe
kuhusu jumbe kwenye magari ya matatu.
Katika sura ya tano, tumetathmini matokeo ya uchunguzi wetu, na pia kutoa mahitimisho na
mapendekezo ya utafiti wa baadaye. | en_US |