dc.contributor.author | Mwangi, Duncan, K | |
dc.date.accessioned | 2021-10-01T12:52:42Z | |
dc.date.available | 2021-10-01T12:52:42Z | |
dc.date.issued | 2005 | |
dc.identifier.uri | http://erepository.uonbi.ac.ke/handle/11295/155581 | |
dc.description.abstract | Tasnifu hii ni uhakiki wa fani katika tamthilia za Kiswahili ambazo zimetungwa na
Warnitila, K.W. Tamthilia hizi ni Wingu La Kupita (1999) na Pango (2003). Katika
tahakiki yetu, tumeteua na kujadili vipengele maalum vya fani. Kazi ina sura tano.
Katika sura ya kwanza, tumeelezea dhana za kimsingi zinazohusiana au kupatikana
katika sorno hili. Dhana hizi ni pamoja na: fani na tamthilia. Tumeelezea pia msingi wa
kinadharia tulioutumia, sababu za kuchagua rnada hii na upeo na mipaka yake.
Tumeweza kurejelea kazi za fasihi zilizowahi kuandikwa zikiangazia fani.
Sura ya pili ni kuhusu ujumla na mjengo wa ploti. Katika sura hii tunaeleza dhana ya
ploti. Vipengele arnbavyo tumejadili ni mfululizo wa vitushi na jinsi vinashirikiana katika
kuleta umoja wa kazi na tumetoa tathmini yetu kuhusu ploti katika kila tamthilia.
Katika sura ya tatu turneshughulikia urnbuji wa wahusika. Tumejadili jinsi wahusika
mbalimbali walivyochorwa katika tarnthilia, nafasi au majukumu yao na mchango
wanaotoa katika uendelezaji wa kazi.
Katika sura ya nne, tumehakiki maturnizi ya lugha katika kazi za Wamitila. Tumeangalia
jinsi lugha irnetumiwa katika mazingira mbalimbali na inavyotumiwa na wahusika wa
urnri rnbalirnbali.Tumejadili pia usanaa na ujumi wa lugha iliyotumiwa.
Sura ya tano ni ya hitimisho na rnapendekezo. Katika sehemu hii tumeangaza
kimukhtasari zile sifa baininifu zinazojidhihirisha katika ujumla wa fani katika kazi za
Wamitila kama tulivyoweza kuzijadili na kuzihukumu. Ubakiki wetu umechambua
udhaifu au ufanifu wa mtunzi katika umbuji wa wahusika na lugha. Tumeweza kutoa
mapendekezo katika tasnifu kuhusu kazi tuliyoifanya. | en_US |
dc.language.iso | other | en_US |
dc.publisher | University of Nairobi | en_US |
dc.rights | Attribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United States | * |
dc.rights.uri | http://creativecommons.org/licenses/by-nc-nd/3.0/us/ | * |
dc.subject | Uhakiki wa fani katlka Tamthilia za K.W.Wamitila. | en_US |
dc.title | Uhakiki wa fani katlka Tamthilia za K.W.Wamitila. | en_US |
dc.type | Thesis | en_US |