Show simple item record

dc.contributor.authorKyalo, Ambrose N
dc.date.accessioned2013-05-03T11:27:35Z
dc.date.available2013-05-03T11:27:35Z
dc.date.issued2006
dc.identifier.citationM.A (Swahili) 2006 Thesisen
dc.identifier.urihttp://erepository.uonbi.ac.ke:8080/xmlui/handle/123456789/18661
dc.descriptionMaster of Arts Thesisen
dc.description.abstractKatika tasnifu hii tumeshughulikia riwaya zaLa peste (1947) ya Albert Camus na Kichwamaji ya Euphrase Kezilahabi. Tumeangaziajinsi waandishi hao wameshughulikia maswala ya udhanaishi na fumbo la Mungu kwa jumla. Uhakiki wetu umegawanywa katika sura tano. Katika sura ya kwanza, tumeelezea tatizo la utafiti, sababu za kuichagua mada hii, mipaka na upeo na yaliyoandikwa kuhusu maswala ya udhanaishi na fumbo la Mungu. Kadhalika tumeelezea msingi wa nadharia iliyotumika katika utafiti huu. Vile vile tumeelezea njia tulizozitumia katika utafiti wetu. Katika sura ya pili, tumeangalia mukhtasari wa riwaya yaKichwamaji, mikinzano iliyomo ya kimitazamo pamoja na dhana ya Mungu. Tumeonyesha jinsi mwandishi wa riwaya hii alivyosawiri swala la udhanaishi na dhana ya Mungu hususan kwa kuzingatia tofauti za kielimu na vizazi. Katika sura ya tatu, tumeshughulikia mukhtasari wa riwaya yaLa peste, mikinzano iliyomo na dhana ya Mungu. Tumeonyeshajinsi mwandishi wa riwaya hii anavyodhihirisha kwamba majanga hasa yanayodhuru afya na kusababisha kifo yanavyoweza kumkengeusha binadamu kutokana na imani katika Mungu. Katika sura ya nne, tumeangazia uchanganuzi-linganishi wa riwaya hizi mbili kuhusiana na mikinzano ya mitazamo. Aidha, tumeangazia dhana ya Mungu katika riwaya hizi mbili. Vile vile, tumeangalia kazi nyingine za fasihi ya Kiswahili ambazo zimeshughulikia maswala ya udhanaishi na fumbo la Mungu. Sura ya tano ni hitimisho na maelezo kuhusu mafanikio na matatizo pamoja na mapendekezo.en
dc.description.sponsorshipUniversity of Nairobien
dc.language.isootheren
dc.titleUdhanaishi na fumbo la Mungu: Uchanganuzilinganishi wakichwamaji (Euphrase kezilahabi) nalapeste (Albert Camus)en
dc.typeThesisen
local.publisherDepatment of Linguistics, University of Nairobien


Files in this item

Thumbnail

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record