Show simple item record

dc.contributor.authorKirabi, Julius M
dc.date.accessioned2021-09-07T09:17:51Z
dc.date.available2021-09-07T09:17:51Z
dc.date.issued2015-11
dc.identifier.urihttp://erepository.uonbi.ac.ke/handle/11295/155441
dc.description.abstractLengo la utafiti huu lilikuwa ni kutathmini na kuchanganua makosa ya kimofosintasia katika lugha ya kimaongezi kwa wanafunzi na walimu katika kaunti ndogo ya Kangema. Walimu na wanafunzi tuliojihusisha nao walikuwa ni wakazi wa eneo hilo na lugha yao ya kwanza ilikuwa ni Kikuyu. Tulitumia mtazamo wa Uchanganuzi Makosa. Nadharia ya uchanganuzi Makosa iliasisiwa na corder na wenzake mnamo mwaka wa 1960. Kwa mujibu wa nadharia hii makosa husababishwa na visababishi vingi mbali na athari ya lugha ya kwanza. Nadharia hii vilevile inachangia katika kubaini mikakati ambayo hutumiwa na wanafunzi katika harakati za ujifunzaji wa lugha ya pili na aidha kutambua visababishi vya makosa na hata chanzo cha makosa mengi katika kazi za wanafunzi. Kwa kuongozwa na nadharia hii basi, katika utafiti wetu, tuliyasikiliza makosa na kuyaandika, kisha tuliyapanga kulingana na aina na hatimaye kuelezea kilichosababisha makosa hayo. Kabla ya kuingia nyanjani na kufanya utafiti wetu tulikisia kwamba makosa mengi ya kimofosintaksia yanayofanyika ni makosa ya kimatamshi. Tulikuwa pia tumetabiri kuwa, makosa mengi ya kimofosintaksia hutokana na mazingira na athari za lugha ya kwanza za wazungumzaji wa Kiswahili katika kaunti ndogo ya Kangema. Vile vile tulikisia kwamba ukiushi wa kimofosintaksia katika matumizi ya lugha hujitokeza pale walimu wanapowahutubia wanafunzi katika vikao rasmi na kwamba kuna uwezekano wa kuyarekebisha makosa hayo. Tulichagua vikundi viwili vya watafitiwa ambao ni walimu na wanafunzi. Tulichukua sampuli rahisi bila kufuata utaratibu wowote. Baada ya kuyakusanya makosa kutoka kwa watafitiwa wetu, kuyaweka katika kategoria kulingana na aina, tuliweza kudhibitisha makisio ya nadharia tete zetu. Tulifanyia utafiti wetu katika shule za upili na za msingi katika kaunti ndogo ya Kangema. Tulishughulikia mokosa ya kimofosintaksia pekee ingawa katika shughuli za kufanya hivyo tulijadili makosa ya kimofolojia. Hii ni kwa sababu makosa ya kimofosintaksia yanaweza kusababishwa na makosa ya kimofolojia. Tuliushughulikia ukiushi wa kimaongezi. Hatukuchunguza ukiushi wa kimaandishi. Wahusika wetu wa utafiti walikuwa ni wale wanaozungumza lugha ya Kikuyu kama lugha yao ya kwanza.Tulikuja kugudua kuwa mengi ya makosa hayo yalisababishwa na athari za lugha ya kwanza ambayo ni Kikuyu. Makosa hayo yalionekana yakiwa mengi sana katika viwango vya chini vya elimu na kupungua kadri mwanafunzi alivyoendelea na masomo ya kiwango cha juu. Umilisi ulionekana kuongezeka kadri kiwango cha e1imu kilivyoongezeka. Ilikuwa dhahiri kuwa walimu waliongea kwa ufasaha zaidi kuliko wanafunzi ingawa hata wao walifanya makosa hapa na pale.en_US
dc.language.isootheren_US
dc.publisherUniversity of Nairobien_US
dc.rightsAttribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United States*
dc.rights.urihttp://creativecommons.org/licenses/by-nc-nd/3.0/us/*
dc.titleMakosa Ya Kimofosintaksia Katlka Lugha Ya Kimaongezi Dhidi Ya Kanuni Za Lugha Ya Kiswahili Sanifuen_US
dc.typeThesisen_US


Files in this item

Thumbnail
Thumbnail

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record

Attribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United States
Except where otherwise noted, this item's license is described as Attribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United States