dc.description.abstract | Tumefanya Uhakiki wa maudhui na mtindo katika Tikitimaji.Tumeangazia maudhui
mbalimbali na lugha ya kitamathali iliyotumika kuendeleza dhamira na maudhui hayo.
Utafiti wetu ulijikita katika Tikitimaji ila ilipotubidi kutoa mifano tuliangazia kazi
nyingine kwa ufupi sana.Uchanganuzi wetu uliongozwa na nadharia mbili: Uhalisia
uliotuongoza katika uchanganuzi wa maudhui na Umitindo uliotuongoza katika
uchanganuzi wa mtindo.
Katika utafiti wetu tuling'amua ya kwamba, jamii ya Tikitimaji ilikumbwa na
changamoto nyingi ambazo wanajamii wanakabiliana nazo ili maisha yao yaweze
kutengenea.Baadhi ya changamoto hizi ni u-h--a-r-i-b--i-f-u-----na uchafuzi wa mazingira, /.
utelekezaji -wa watoto, udhalimu na unyanyasaji, miundo msingi mibovu na mfumo ----
mbaya wa uchukuzi, umaskini na athari zake, mchango wa vijana katika ujenzi wa jamii <,
mpya na jinsi wanavyoshirikiana na wazee katika suala hili,
Maudhui haya yameendelezwa kwa kutumia lugha yenye mvuto na mnato unaowavutia
wasomaji na kuipa riwaya hii ujumi mwafaka.
Utafiti wetu umegundua kwamba, masuala yanayowakabili wanatikitimaji ni ya kijamii,
kiuchumi na kisiasa ambapo walala heri wanawanyanyasa walala hoi, jambo linalozua
migogoro baina ya makundi haya mawili.Kundi la walala heri linapigania kuendeleza
unyanyasaji nalo la walala hoi likikazana kujikomboa. | en_US |