Show simple item record

dc.contributor.authorMaombe, Jacob O
dc.date.accessioned2021-09-16T11:50:55Z
dc.date.available2021-09-16T11:50:55Z
dc.date.issued2011
dc.identifier.urihttp://erepository.uonbi.ac.ke/handle/11295/155484
dc.description.abstractKatika utafiti huu wa ukombozi wa mwanamke, tumeona kwamba ukombozi wa mwanamke unamtegemea mwanamke mwenyewe. Mwanamke anafaa kuchukua mstari wa mbele ili kupigania haki zake za kijamii kama njia ya kupinga ugandamizwaji anaotendewa na mwanamume. Ili kutimiza haya inafaa mwanamke ajikomboe katika hali zote za maisha kama vile: kijamii, kiuchumi na kisiasa. Anapofikia hali hii, mwanamke ataweze kujitegemea katika utendakazi na kuchukua uamuzi wa busara katika jamii. Kufanya hivi kutaweza kumwondolea majaribio yanayolenga kumgandamiza. Katika utafiti huu tumeweza kuonyesha namna wahusika wa kike katika riwaya za Habwe wamejishughulisha na harakati mbalimbali zinazolenga kuwakomboa kutokana na ugandamizaj i wa wanaume. Katika sura ya pili tumeweza kutaja baadhi ya riwaya zingine za mwandishi ambazo kwa ujumla zinanuia kuleta heshima, haki, usawa na ushirikiano katika jimii. Aidha tumeweza kujadili hali mbalimbali za ukombozi wa kijamii, kiuchumi na kisiasa. Tumejadili kuhusu dhuluma wanazopitia wanawake kutoka kwa wanaume. Baadhi ya dhuluma hizi ni: kupewa adhabu kali, kulazimishwa katika ridoa, kubaguliwa katika urithi, kubaguliwa katika taasisi za elimu na kubaguliwa katika uongozi. Ugandamizaji huu hutekelezwa na vyombo vya kijamii kama vile: Utamaduni ndoa na dini. Katika sura ya tatu na ya nne tumejadili kuhusu harakati za kujikomboa dhidi ya dhuluma za mwanaume. Kupitia riwaya ya Maumble sf Huja. Tumeonyesha naruna mwanamke amejiimarisha kiuchumi na kijamii lakini kwa kiasi kikubwa kwa kutegemea nguvu za vi mwanamume. Riwaya hii imeonyesha mwanzo tu wa harakati za ukombozi ambapo mwanamke amejikomboa kwa kiasi kidogo. Kwa kutumia mali ya mwanamume, mwanamke amejianzishia miradi ambayo imefanikiwa japo kwa kiasi kidogo. Riwaya ya Fumbo la Maisha, mwanarnke ameweza kujikomboa kiuchumi, kijamii na kisiasa. Amedhihirisha hayo wazi kwa kuanzisha miradi yake ya kiuchumi kama vile biashara, kilimo, na ufugaji. Hatimaye amefikia upeo wa kudai na kupewa haki zake kama vile ardhi haki ya kuiongoza jamii kwa kuchaguliwa mbunge.en_US
dc.language.isootheren_US
dc.publisherUniversity of Nairobien_US
dc.rightsAttribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United States*
dc.rights.urihttp://creativecommons.org/licenses/by-nc-nd/3.0/us/*
dc.subjectUkombozi Wa Mwanamkeen_US
dc.titleUkombozi Wa Mwanamke Katika Riwaya Za Habween_US
dc.typeThesisen_US


Files in this item

Thumbnail
Thumbnail

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record

Attribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United States
Except where otherwise noted, this item's license is described as Attribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United States