dc.description.abstract | Tasnifu hii inahusu dhana ya uchimuzi katika uendelezaji wa riwaya ya kimajaribio au mpya ya
Mafamba (2008). Ni riwaya ya kwanza ya Olali inayomulika hali ya kisiasa katika jamii yetu na
harakati za wananchi za kuwang'oa viongozi wadhalimu. Katika kuitafiti kazi hii, tuliongozwa
na mwelekeo wa kihakiki wa Urasimu wa Kirusi.
Utafiti huu unahusu nafasi ya uchimuzi katika nwaya ya Mafamba. Suala ambalo
tumeshughulikia kwa kuangazia uchimuzi katika ngazi ya wahusika na matumizi ya lugha.
Utafiti huu ulilenga kudhihirisha kuwa, uchimuzi ni nguzo kuu katika uendelezaj i wa riwaya ya
kimajaribio au mpya ya Mafamba.
Tumeigawa tasnifu hii katika sura tano. IIi kufikia malengo yetu, sura ya kwanza
imeshughulikia utangulizi kwa ujumla. Utangulizi huu unahusu usuli wa mada, tatizo la utafiti,
madhumuni ya utafiti, nadharia tete. sababu za kuchagua mada, mipaka na upeo. misingi ya
kinadharia, yaliyoandikwa kuhusu mada yetu na njia za utafiti.
Katika sura ya pili, tumezungumzia msuko wa riwaya ya Mafamba ambao unajenga msingi wa
uelewa wa riwaya hii. Tumeiona riwaya hii kuwa ya kuvutia na kusisimua hasa kutokana na
usimulizi wake unaoelezea masuala nyeti ya kisiasa ya jamii yetu katika mtindo mpya wa
uandishi kwa njia inayokiuka sifa za uandishi wa riwaya za jadi.
Katika sura ya tatu tumeshughulikia uchimuzi katika kiwango cha wahusika. Uchimuzi huu
unatokea katika kiwango cha maana au kisemantiki. Tumebainisha kwamba, uchimuzi wa
wahusika katika riwaya ya Mafamba unabainika kupitia kwa usawiri wao kiasi cha kubatilisha
dhana nzima ya uhusika hata ingawa matendo yao na wasifu wao unachukuana na hali ya kisasa
ya maisha ya jamii yetu kwa jinsi tunapata kuwatambua, kutambua tabia zao na mielekeo yao.
xi
Aidha kupitia kwa uchimuzi katika kiwango hiki, dhamira ya mwandishi na aidha maudhui
katika riwaya hii yanabainika.
Sura ya tatu inahusu uchimuzi katika kiwango cha matumizi ya lugha. IIi kufanikisha lengo letu,
tuliangazia vipengele vya matumizi ya lugha katika kiwango cha kimsamiati na kisemantiki.
Utafiti wetu umebaini kuwa, viwango hivi vinachimuza sifa zilizozungumziwa na Wana-
Urasimu kama uajinabishaji au kufanya kazi ya kifasihi kuonekana kuwa ngeni, matumizi ya
mbinu kadha za uwasilishaji na matumizi ya kipekee ya lugha.
Sura ya tano inahusu hitimisho la utafiti. Katika sehemu hii, tumerejelea mada ya utafiti huu na
maswala ya kimsingi tuliyoyaelezea katika sura ya kwanza. Kutokana na matokeo ya
uchanganuzi data yetu, tumerejelea nadharia tete zetu ili kuzikubali na pia tumetoa mahitimisho
na mapendekezo ya utafiti wa baadaye. | en_US |