dc.description.abstract | Kazi hii inahusu uchanganuzi wa Kauli katika sentensi elekezi ya Kiswahili sanifu kwa
kutumia nadharia ya Ubanifu. Kazi yenyewe ilikuwa na malengo ya kueleza dhana ya
uambishaji na kuonyesha viambishi vya kauli katika kitenzi cha Kiswahili sanifu. Aidha, kazi
hii imelenga kuonyesha uhusiano uliopo kati ya yambwa na viambishi vya kauli katika
sentensi elekezi ya Kiswahili sanifu.
Kazi hii imefaulu katika kuonyesha kuwa dhana za uambishaji na unyambuaji ni taratibu
mbili tofauti za kisarufi, na kwamba viambishi vya kauli ni tokeo la uambishaji wala sio la
unyambuaji. Utafuti huu umebainisha kwamba viambishi vya kauli sio tu viambishi tamati,
bali pia huongozwa na kanuni mbalimbali ikiwemo kanuni ya wiano wa irabu. Utafiti huu
umeonyesha pia kwamba, Usogezi kama mojawapo ya mihimili mikuu ya nadahria ya
Ubanifu, huongozwa na kanuni mbalimbali za iktisadi kwa Iengo la kufanikisha ukuaguzi wa
sifa muhimu.
Kazi yenyewe imepangwa katika sura tano; kila sura ikishughulikia vipengele mahususi.
Sura ya kwanza imetoa utangulizi wa jumla kuhusu dhana za kauli na sentensi elekezi. Aidha
sura hii imefafanua tatizo 1a utafiti, madhumuni ya utafiti, nadharia tete zilizoongoza utafiti
pamoja na kueleza sababu za kuchagua mada ya utafiti. Sura hii pia imebainisha upeo na
mipaka ya utafiti kabla ya kufafanua msingi wa nadharia iliyotumiwa ya Ubanifu na
kudurusu yaliyoandikwa kuhusu kauli na nadharia ya Ubanifu. Hatimaye, sura hii imeeleza
mbinu za utafiti na umuhimu wa utafiti huu. Sura ya pili imeshughulikia dhana za uambishaji
na unyambuaji na kutoa vigezo vitano vya kuzitofautisha. Aidha, sura hii imeangazia
viambishi awali na tamati vya vitenzi vya Kiswahili sanifu kwa kina.
Katika sura ya tatu, vitenzi vya Kiswahili vimefafanuliwa kwa kuonyesha aina zake kwa
misingi mitatu. Sura hii imehitimishwa kwa kuangazia kauli mbalimbali za vitenzi vya
Kiswahili katik a muktadha wa sentensi elekezi. Sura ya nne imejishughulisha na uchanganuzi
wa data 'yetu ambapo kauli tisa za vitenzi zimeelezwa kwa kutumia nadharia ya ubanifu.
Dhana za uhusika I1J v.ilcnsi pia zimeshughulikiwa hapa. Sura hii imetathmini kwa kina
nafasi ya kanuni mbat i.nbali za nadharia ya Ubanifu zinazohakikisha kuwa tungo
zinazozalika zinakuwa sahihi sio tu kifonetiki, bali pia kimantiki. Sura ya tano ya tasnifu hii
imetoa mahitimisho ya utafiti wetu. Zaidi ya mahitimisho, sura hii imetoa mapendekezo
ambayo watafiti wenginc wanaweza kuzingatia katika tafiti zao za baadaye. | en_US |