Show simple item record

dc.contributor.authorKofa, Tola
dc.date.accessioned2021-09-30T08:40:02Z
dc.date.available2021-09-30T08:40:02Z
dc.date.issued2009
dc.identifier.urihttp://erepository.uonbi.ac.ke/handle/11295/155562
dc.description.abstractFani ni jumla ya vipengele vya kimtindo au kisanaa vinavyotumiwa kuwasilisha ujumbe. Katika tenzi vipengele vinavyojitokeza ni mtindo, muundo, toni, msuko, mandhari, wahusika, wakati, matumizi ya lugha na vipengele vingine vya kisanaa. Tumeigawanya tasnifu hii katika sura nne. Sura ya kwanza inaeleza dhamira yetu kwa kufafanua dhana za somo la utafiti, madhumuni ya utafiti, sababu ya kuchagua somo, yaliyoandikwa kuhusu somo, upeo na mipaka, msingi wa nadharia, nadharia tete na njia za utafiti. Sura ya pili inachanganua dhana ya fasihi simulizi, maana ya ushairi, chimbuko la ushairi, maendeleo ya ushairi, athari za wageni, mashairi huru na lugha ya ushairi.Sura ya tatu inafafanua vipengele vya kimtindo, matumizi ya lugha na vipengele vya kisanaa. Sura ya nne inafananua nadharia tete tano. Kwa ufupi, nadharia tete ya kwanza inasema kuwa mtunzi ametumia msamiati akilenga hadhira ya kisasa. Maneno kama keshi (20), saini (204), baiskeli na motukari (277) n.k ni maneno yanayotuonyesha taathira za msamiati wa Kiingereza. Hawa ndio wageni waliofika mwisho baada ya Wareno na Waarabu ambao athari zao pia zinapatikana kwenye msamiati wa watu wa Kilwa. Neno malaya la Kiswahili lina asili ya neno malay la Kireno, yaani mtumishi wa kike anayetoka nchini Malay. Neno mvinyo la Kiswahili limetoholewa kutokana na neno vinho la Kireno. Pia neno msabiki (24), akaqimu (42) n.k ni maneno yaliyotoholewa kutokana na msamiati wa Kiarabu, Kwa hivyo, mvurugo huo ulioikumba lugha ya ushairi wa Kiswahili unadhihirisha kuwa hadhira hii imeingiliana na wageni kabla ya, wakati wa na hata baada ya uhuru. Bali hii ya maingiliano inadhihirishwa kutokana na utohozi wa msamiati wa wageni; hii ina maana kuwa hadhira hii ni ya kisasa. Ya pili inasema kwamba baadhi ya wahusika hubadilisha toni kulingana na hadhira. Anapoongea na wachawi wenzake, Shambi hutusi, hukaripia na huarnrisha.en_US
dc.language.isootheren_US
dc.publisherUniversity of Nairobien_US
dc.rightsAttribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United States*
dc.rights.urihttp://creativecommons.org/licenses/by-nc-nd/3.0/us/*
dc.subjectUhakiki Wa Fani, Swifa Ya Nguvumalien_US
dc.titleUhakiki Wa Fani Katika Utenzi Wa Swifa Ya Nguvumalien_US
dc.typeThesisen_US


Files in this item

Thumbnail
Thumbnail

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record

Attribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United States
Except where otherwise noted, this item's license is described as Attribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United States