Show simple item record

dc.contributor.authorNyarunda, Hyline M
dc.date.accessioned2023-03-22T06:13:44Z
dc.date.available2023-03-22T06:13:44Z
dc.date.issued2022
dc.identifier.urihttp://erepository.uonbi.ac.ke/handle/11295/163304
dc.description.abstractUtafiti huu ulinuia kuchunguza athari za ulumbilugha kwa Kiswahili. Tasnifu hii imegawanywa kwa sura tano. Katika sura ya kwanza tulishughulikia utangulizi wa kazi hii kwa ujumla kwa kuangazia tatizo la utafiti, maswali na malengo ya utafiti huu, sababu za kuchagua mada, yaliyoandikwa kuhusiana na mada yetu na vile vile mbinu za utafiti. Katika sura ya pili, tulishughulikia dhana za ulumbilugha na kuchanganya ndimi na hatimaye tuliangazia mielekeo ya wanafunzi kuhusu Kiingereza, Kiswahili na Sheng‟. Tulijikita kwa athari hasi na chanya za Sheng‟ na Kiingereza kwa Kiswahili kwa kuangazia insha za wanafunzi wa shule za msingi za CGHU na Moi Avenue. Kutokana na data ya utafiti huu, tuligundua kuwa athari hasi ni nyingi zaidi ya athari chanya na hili ni jambo linalowafanya wanafunzi wa shule za msingi za CGHU na Moi Avenue kupata alama za chini katika uandishi wa insha za Kiswahili. Tulishughulikia athari hasi na chanya za sheng‟ na Kiingereza kimofolojia katika sura ya tatu na vile vile kisintaksia katika sura ya nne. Athari hasi za Sheng‟ na kimofolojia ambazo tulishughulikia ni: ukataji wa silabi za Kiswahili kwa namna isiyofaa, kuandika ukubwa na udogo wa nomino za Kiswahili visivyo na pia kunyambua vitenzi vya Kiswahili visivyo. Athari hasi za Kiingereza tulizobaini katika mofolojia ni uswahilishaji maneno ambayo yana msamiati uliozoeleka katika Kiswahili, matumizi ya konsonanti za Kiingereza katika uandishi wa insha, kutumia maneno ya Kiingereza na uambishaji wa maneno ya Kiswahili visivyo. Athari chanya ya ulumbilugha kimofolojia iliyobainika katika data ya utafiti huu ni ufahamu wa maana za maneno. Katika sintaksia, tulishughulikia athari hasi na chanya za ulumbilugha katika uandishi wa insha za Kiswahili. Tuliangazia sentensi katika insha za watafitiwa wetu na tuligundua kuwa athari hasi za Sheng‟ kisintaksia ni: matumizi ya mbinu ya uhuishaji pasipofaa, uongezeaji wa viambishi visivyo, kuendeleza misamiati ya Kiswahili visivyo na matumizi ya maneno ya Sheng‟. Tulibaini kuwa pia umilisi wa Kiingereza uliwaathiri kwa njia hasi kwa kuwa wanafunzi wa shule za msingi za CGHU na Moi Avenue wanaendeleza viambishi vya nafsi visivyo, matumizi mabaya ya vivumishi vya aina mbalimbali kama vile vivumishi vya a-unganifu, vionyeshi, vimilikishi, virejeshi na vile vya idadi. Athari hizi hasi zinaifanya sentensi kutokuwa sahihi na hivyo basi wanafunzi wanaadhibiwa kwa kufanya makosa ya kisarufi. Hatimaye, tulishughulikia athari chanya za ulumbilugha kisintaksia na tulibaini kuwa uliwawezesha wanafunzi wa shule za msingi za CGHU na Moi Avenue wanatunga sentensi ambazo zimekamilika kimaana, sahihi na kimantiki. Hatimaye tulishughulikia mahitimisho ya utafiti huu na mapendekezo kwa watafiti wa baadaye.en_US
dc.language.isoenen_US
dc.publisherUniversity of Nairobien_US
dc.rightsAttribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United States*
dc.rights.urihttp://creativecommons.org/licenses/by-nc-nd/3.0/us/*
dc.subjectUlumbilugha Na Athari Zake Katika Uandishi Wa Inshaen_US
dc.titleUlumbilugha Na Athari Zake Katika Uandishi Wa Insha Za Shule Za Msingi Ya Cghu Na Moi Avenue; Kifani Cha Sheng Na Kiingereza Kwa Kiswahilien_US
dc.typeThesisen_US


Files in this item

Thumbnail
Thumbnail

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record

Attribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United States
Except where otherwise noted, this item's license is described as Attribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United States