Ukiushi katika lugha ya kimaongezi dhidi ya kanuni za kiswahili sanifu
Abstract
Utafiti . huu umetokanana imani kwamba ukiushi katika lugha ya kimaongezi ni tukio halisi na dhahiri katika matumizi ya lugha yo yote ile. (Taz. Max Black, 1968).
Kuifahamu lugha na kuielewa kikamilifu kunahusu pia ufahamu wa hali ya ukiushi na sababu za ukiushi huo unaotoka.
Tasnifu hii imechunguza na kuonyesha baadhi ya makosa (ukiushi) yanayotokea katika hali halisi ya maongezi ya wahusika kutoka katika mtaa wa Kariobangi South, mjini
Nairobi. Kazi hii imegawanywa katika sura sita.
Kila sura inajadili kipengee maalum kinachohusu matumizi ya lugha.
Kila sura ina utangulizi, na panapo hitajika, iishio kinachotoa muhtasari na uamuzi wa jumla kulingana na matokeo ya utafiti. Sura ya kwanza ni utangulizi wa utafiti. Utangulizi
wa sura hii unatoa maelezo machache kuhusu mtaa wa Kariobangi South (tulikofanyia utafiti) na wakazi wake. Katika sura hii pia tumejadili somo letu la utafiti,
madhumuni yetu ya kuufanya utafiti huu na upeo wa tasnifu. Zaidi ya hayo pia 'tumeelezea kuhusu nadharia tunayoitumia kama kigezo cha kupirnia matumizi ya lugha. Katika sehemu ya 'Yaliyofanywa kuhusu somo', tunajadili baadhi ya kazi zingine zilizofanywa na kuandikwa na ambazo, kwa namna
Citation
Master of ArtsPublisher
University of Nairobi Department of Kiswahili