Sintaksla ya virai vya kiswahili sanifu na kikikuyu cha kabete - ulinganishi
Abstract
Lengo la kazi hii ni kulinganisha miundo ya virai baina ya Kiswahili sanifu na Kikikuyu cha Kabete. Hii ni kwa kutumia nadharia sanifu ya Sarufi Geuzi Maumbo Zalishi kulingana na Chomsky (1965) 'Aspects of the Theory of Syntax'.
Tumegawanya kazi yetu katika sehemu tano. Sura ya kwanza ni utangulizi ambapo tunapata mada yenyewe na msingi wa lugha zote mbili yaani Kiswahili sanifu na Kikikuyu cha Kabete. Katika sura ii pia tumethibitisha kuwa Kikikuyu sanifu ndicho Kikikuyu cha Kabete. Mambo mengine yaliyoshughulikiwa katika sura hii ni sababu za kulichagua somo hili, upeo na mipaka, udurusu wa maandishi, nadharia tete na njia za utafiti.
Sura ya pili infafanua dhana ya virai na kisha kuchanganua miundo ya virai vya Kiswahili sanifu. Miundo hii imechanganuliwa kwa kutumia nadharia sanifu.
Sura ya tatu inahusu uchanganuzi wa miundo ya virai katika Kikikuyu cha Kabete. Hii ni kwa kuzingatia nadharia sanifu ya SGMZ.
Sura ya nne inahusu ulinganishi wa miundo ya virai baina ya Kiswahili sanifu na Kikikuyu cha Kabete. Sura hii inaelezea kufanana na kutofautiana katika miundo ya virai. Sura hii pia inaelezea kaida ya nadharia sanifu na kuonyesha ikiwa miundo ya virai katika Kiswahili sanifu na Kikikuyu cha Kabete inakaidi sintaksia ya nadharia sanifu.
Citation
Master of ArtsPublisher
University of Nairobi. Department of Linguistics and Languages