dc.description.abstract | Matlaba ya tasnifu hii ni kufanya uehanganuzi wa kiufafanuzi wa kikundi nomino eha Kiswahili kwa kutumia nadharia ya sintaksia ya 'X-Bar' Katika kiolezofaridi eha nadharia ya sarufi geuzamaumbo sanifu panuzi.
Tumeibawibu kazi hii katika sura tano. Katika sura ya kwanza, tunatoa maelezo ya kimsingi yanayohusu kikundi nomino eha Kiswahili. Aidha, sura hii inaeleza somo la utafiti, madhumuni ya utafiti na upeo wa tasnifu. Mambo mengine ambayo yanaangaliwa ni pamoja na sababu za kuliehagua somo, kikundi nomino kikiwa ni maarubu yetu, nadharia tete, yaliyoandikwa kuhusu
somo hili, msingi wa nadharia na njia za utafiti.
Sura ya pili inaehunguza mofolojia ya nomino ya Kiswahili. Unyambuaji na uambishaji ni dhana zinazopewa nafasi kubwa katika sehemu hii. Ngeli za nomino zinaehanganuliwa na upatanisho uliopo.
Sura ya tatu inahusu uvumishaji wa nomino na kategoria tofauti za kisintaksia zinazohusiana na kikundi nomino. Kiini eha sura hii kiliangaza, hususan, maneno mbalimbali yanayovumisha nomino katika lugha ya Kiswahili.
Sura ya nne inachunguza kwa tafsili kikundi nomino eha Kiswahili. Mifumo miwili ya kuwakilisha miundo ya kategoria inatumika. Mifumo hiyo ni kiunzi
eha sarufi muundo virai na kiunzi eha 'X-bar'.
Hata hivyo mfumo wa sarufi muundo virai ulitumika tu kama msingi na kitangulizi cha sintaksia ya X-bar ambayo tumeitumia kukiehanganua kikundi nomino eha Kiswahili.
Sura ya tano ni hitimisho jumuishi ambapo matokeo ya utafiti wetu yanaelezwa. Nadharia tete zetu zinaangaliwa na mapendekezo yanatolewa kuhusiana na kipengele eha sintaksia, hususan kikundi nomino cha Kiswahili. | en |