Uhakiki Wa Kimaudhui Na Kifani Wa Kidagaa Kimemwozea
Abstract
Tasnifu hii ilishughulikia uhakiki wa kifani na kimaudhui wa Kidagaa Kimemwozea ya Ken
Walibora(2012). Tuliangalia maudhui na tulinuia kuonyesha mbinu zilizotumiwa katika
kuwaumba wahusika na jinsi wahusika vijana walivyopigania kuondoa ukoloni mambo leo
katika nchi ya Tomoko. Pamoja na hayo tulishughulikia nadharia tete ya uhakiki ambayo ni
mhimili wa utafiti huu. Sababu za kuchagua mada pia zimeelezwa. Kazi yetu iliangazia
maudhui, fani na wahusika. Kwa vile kuna njia nyingi za kuwasiri wahusika sisi tumejibana kwa
wahusika wakuu, wasaidizi na wajenzi.
Misingi ya nadharia za uhalisia wa kijamaa na umuundo imezingatiwa katika uhakiki wetu.
Nadharia ya uhalisia wa kijamaa ni kwa mujibu wa wanafalsafa kama vile George Lukacs,
Marxim Gorky, Zandnov na wengineo.
Nadharia ya umuundo ni kwa mujibu wa Ferdinand De Saussure. Nadharia hii kuchunguza
vipengele vya kazi ya sanaa, jinsi vinavyohusiana hadi kuikamilisha kazi hiyo. Huangalia
namna sehemu mbalimbali za kazi ya sanaa zimefungamana. Mbinu za utafiti tulizotumia ni za
maktabani ambapo tulirejelea makala mbalimbali yakiwemo majarida, tasnifu na vitabu kadha
wa kadha.
Publisher
University of Nairobi Department of Linguistics
Description
Tasnifu hii imetolewa ili kutosheleza baadhi ya mahitaji ya
shahada ya uzamili katika Chuo Kikuu cha Nairobi