Show simple item record

dc.contributor.authorMirianga, Rose Kaumeuru
dc.date.accessioned2014-11-25T12:02:23Z
dc.date.available2014-11-25T12:02:23Z
dc.date.issued2014
dc.identifier.urihttp://hdl.handle.net/11295/75310
dc.descriptionThesis MAen_US
dc.description.abstractNchini Kenya, walimu wa shule za msingi ni kielelezo cha kuigwa na wanajamii walio wengi hasa katika maeneo ya mashambani. Aghalabu, wanayoyatenda na wanayoyasema walimu hawa kuhusiana na lugha ndiyo yanayofuatwa na wanajamii walio wengi. Tasnifu hii ni uchunguzi wa mielekeo ya wadau hawa muhimu kuhusu majukumu yaliyotengewa lugha mbalimbali, ukuzaji na uendelezaji wa matumizi ya lugha kama inavyoangaziwa na kauli za Katiba ya Kenya zihusuzo suala la lugha. Mielekeo ya wadau hawa inatarajiwa kuwa mwongozo kwa waundaji sera ya lugha na pia wapangaji lugha ili kubuni mikakati ya kuhimiza ushawishi na uhusika wa walimu husika, kama wadau muhimu, katika kutekeleza sera ya lugha kama inavyojitokeza katika Katiba ya Kenya ya mwaka wa 2010. Uchunguzi huu ulijikita nyanjani ambapo data ilikusanywa kwa njia ya hojaji, mahojiano na utazamaji wa tabia za watafitiwa kuhusu lugha ya Kiswahili, Kiingereza na lugha asilia (Kimeru). Kutokana na matokeo ya utafiti huu, mielekeo ya watafitiwa kuhusu suala la lugha kama linavyojitokeza katika Katiba ya Kenya, imetokana na masiala ya kihistoria, kijamii, kiisimu na kiuchumi. Uchanganuzi wa data ya utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Kijamiinafsia iliyoasisiwa na Lambert (1963) na ile ya Kijamii ya Fishman (1972).en_US
dc.language.isoenen_US
dc.publisherUniversity of Nairobien_US
dc.titleMielekeo ya walimu wa shule za msingi kuhusu suala la lugha kama linavyoelezwa katika katiba ya Kenyaen_US
dc.typeThesisen_US
dc.type.materialen_USen_US


Files in this item

Thumbnail

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record