Show simple item record

dc.contributor.authorKaroki, Emaitta
dc.date.accessioned2014-11-27T12:42:58Z
dc.date.available2014-11-27T12:42:58Z
dc.date.issued2014
dc.identifier.urihttp://hdl.handle.net/11295/75505
dc.description.abstractUtafiti huu unahusu suala la uhamaji na uhamiaji kama linavyoendelezwa katika riwaya ya kitawasifu ya Mbali na Nyumbani iliyoandikwa na Adam Shafi. Suala la uhamaji na uhamiaji ndilo lililotawala riwaya nzima kutoka mwanzo hadi mwisho. Mwandishi wa riwaya hii ameathiriwa na suala hili la uhamaji na uhamiaji kwani ameyapitia hayo yote. Hii ndiyo sababu riwaya yenyewe inaitwa ya kitawasifu. Uhakiki wetu umeongozwa na nadharia ya uhalisia ambayo hujikita katika utoaji wa picha halisi ya maisha ya binadamu. Nadharia hii ina vipengele vingi lakini sisi tumetumia vipengele vitatu. Hivi ni: Kipengele cha kihistoria, kisiasa na kitamaduni. Kazi hii imelenga kushughulikia tatizo la utafiti ambalo linahusu uhamaji na uhamiaji. Matatizo yanayowakumba wanajamii katika sehemu mbalimbali za ulimwengu hasa mataifa ya ulimwengu wa tatu ndiyo yaliyotusukuma kufanya utafiti huu. Matatizo haya yanazidi kuangaziwa kila uchao kupitia vyombo mbalimbali vya habari. Aidha, tumechambua maudhui yanayoingiliana na suala la uhamaji na uhamiaji katika riwaya husika. Sababu yenyewe ni kwamba, maudhui hayo yanachangia katika kuboresha au kufanya maisha ya wahusika kuwa magumu wakiwa katika hali ya uhamaji na uhamiaji. Si hayo tu bali tumefafanua aina za uhamaji na uhamiaji zinazopatikana katika riwaya yenyewe. Vilevile, tumeangalia sababu zinazochangia hali hiyo na manufaa ya uhamaji na uhamiaji. Zaidi ya hayo, tumeeleza kwa kina matatizo yanayowakumba wahusika katika riwaya hii na jinsi wanavyojaribu kuyatatua. Katika utafiti huu, tumegundua kuwa matatizo yanayowakumba wahusika katika riwaya hii ni yaleyale yanayowakumba watu wengine wakiwa katika hali ya uhamaji na uhamiaji popote pale. Baada ya kupata hayo, tunapendekeza kwamba, serikali na mataifa yaliyokumbwa na tatizo hili yajaribu kuweka mikakati ya kuchunguza kiini chake na kutafuta njia za kulitatua kabla halijaharibu mishikamano ya wanajamii.en_US
dc.language.isoenen_US
dc.titleSuala la uhamaji na uhamiaji kama linavyoendelezwa katika riwaya ya Mbali na Nyumbani ya Adam Shafien_US
dc.typeThesisen_US
dc.type.materialen_USen_US


Files in this item

Thumbnail

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record