Show simple item record

dc.contributor.authorNjoroge, Florence W
dc.date.accessioned2014-12-02T11:04:26Z
dc.date.available2014-12-02T11:04:26Z
dc.date.issued2014
dc.identifier.citation(M.A) Kiswahili katika Chuo Kikuu cha Nairobi. Idara ya Kiswahili, Chuo Kikuu cha Nairobi.en_US
dc.identifier.urihttp://hdl.handle.net/11295/75919
dc.description.abstractSheng imekuwa moja wapo wa lugha vipindi ambayo inatumika sana kwenye miji mingi nchini Kenya ukiwemo mji wa Nakuru. Matumizi ya lugha hii nyumbani, mitaani na hata shuleni umepelea lugha hii kukua na hata kuongeza misamiati na kuongezeka kwa watumiaji wa lugha hii. Utafiti huu ulilenga kutambulisha hali, hadhi na majukumu ya Sheng mjini Nakuru huku tukilinganisha Sheng na lugha nyingine zinazotumika mjini humo. Sababu ya kuteua mada hii ni kuona kuwa vijana wengi mijini wanatumia Sheng kama kitambulisho chao kilugha na haijatambulika kisheria. Malengo ya kazi hii nikutafiti kama Sheng ina majukumu maalum mjini Nakuru, kama hadhi ya lugha hii ni ya chini na kama kuna tofauti zilizoko katika matumizi ya Sheng kimaeneo. Ukusanyaji wa data kwa ajili ya utafiti huu ulifanywa kwa njia ya hojaji ambayo iliyafumbata maswala ambayo kwa kawaida hupelekea mtuamiaji wa lugha kuonekana kana kwamba ni mtu aliye na uelewa wa lugha tofauti mbali na kuonyesha hadhi zipewazo lugha mjini Nakuru. Uchanganuzi wa data ulifanywa kwa kutumia nadharia ya lugha na utambulisho wa jamii ya Gumperz na Cook (1982), nadharia chanzo cha ujifunzaji wa lugha ya pili ya Stephen Krashen (1989) na nadharia ya jumuishi na utambulisho ya Gile (1979). Uchanganuzi kutokana na nadharia hizi umeonyesha kuwa kila lugha huhusishwa na kikundi fulani cha wahusika na lugha hii huwa kama kitambulisho cha jamii husika. Kila lugha hupewa majukumu na hadhi kulingana na watumizi wake ni kina nani. Mbinu za ujifunzaji lugha pia huchangia katika kuipa lugha fulani majukumu na hadhi ya lugha husika. Sheng ni lugha ambayo ni kitambulisho cha vijana wa mijini nchini Kenya ukiwemo mji wa Nakuruen_US
dc.language.isoenen_US
dc.publisherUniversity of Nairobien_US
dc.titleHali, Hadhi Na Majukumu Ya Sheng Mjini Nakuruen_US
dc.typeThesisen_US
dc.type.materialen_USen_US


Files in this item

Thumbnail

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record