Show simple item record

dc.contributor.authorGikambi, Hezekiel P
dc.date.accessioned2015-12-09T12:13:45Z
dc.date.available2015-12-09T12:13:45Z
dc.date.issued2015
dc.identifier.urihttp://hdl.handle.net/11295/93216
dc.descriptionThesisen_US
dc.description.abstractUtafiti wa lugha kuegemea mitazamo ya kikompyuta umetamalaki katika lugha zilizoendelea kidijitali kama Kiingereza na nyinginezo ila dhana hii haijakita mizizi kabisa katika utafiti wa lugha za Kiafrika kama Kiswahili. Utafiti huu umeangazia suala la matumizi ya teknolojia ya lugha katika utafiti wa Kiswahili kwa kuchunguza na kutathmini mbinu mbali mbali zilizotumika katika mradi wa SALAMA (Swahili Language Manager), ulioasisiwa na Arvi Hurskainen profesa wa taaluma za lugha za Kiafrika katika Chuo Kikuu cha Helsinki nchini Finland kutoka 1985- 2015 ili kutambua ukweli wa hali ya utafiti wa Kiswahili katika jukwaa la teknolojia ya lugha. Kwa kutumia mazingira ya SALAMA, ambayo yalishughulikia Kiswahili na kuchunguza nyanja zake mbali kwa kutumia programu zilizojengwa kwenye misingi ya kanuni za lugha na za kikompyuta, utafiti huu ulilenga kubainisha mbinu mbalimbali zilizohusika katika utafiti wa kikompyuta wa lugha ya Kiswahili katika mradi huu na kuzichunguza mbinu hizo zilizotumika kufanyia utafiti na kuchanganulia vipengele tofauti tofauti vya lugha hii, na iwapo zinaweza kuwa zimechangia katika kukuza na kuendeleza utafiti wa Kiswahili kama lugha ya Kiafrika inayoweza kutafitiwa kwa kutumia Teknolojia ya Lugha au Uhandisi Lugha. Katika kufanya hivi, Utafiti umelenga kuonyesha umuhimu, uamilifu na utumiwaji wa kongoo au kopasi katika Teknolojia ya Lugha na jinsi kanzi hii inavyoweza kuboresha utafiti katika lugha ya Kiswahili kikompyuta. Nadharia ya Msambao wa Ugunduzi (Diffusion of Innovation Theory) iliyoasisiwa na Everett Rogers (2003) pamoja na Nadharia ya Isimu Kongoo au Mtazamo wa Kikongoo zimetumika katika kujaribu kueleza jinsi teknolojia ya lugha ni mkabala ulio na manufaa zaidi kiutafiti kuliko mbinu za kimapokeo. Kupitia kwa data kutoka kwa hojaji na mifano kutoka kwa ripoti mbali mbali na kazi za kitaaluma zinazohusu SALAMA, utafiti umebaini kuwa teknolojia ya lugha inachangia katika utafiti ya kiujarabati zaidi, ina uwezo wa kuichakata data kubwa zaidi kikompyuta kuliko uwezo wa binadamu, inampa mtafiti mnepo na uhuru zaidi, inahifadhi lugha kikompyuta na inaweza kushughulikia lugha ya Kiswahili kiutafiti katika maeneo yote kutoka uundaji na utathmini wa kamusi, tafsiri-mashine, uchanganuzi wa kimofolojia, kisintaksia,kisemantiki,ufundishaji lugha na miongoni mwa masuala mengine.en_US
dc.language.isoenen_US
dc.publisherUniversity of Nairobien_US
dc.titleTeknolojia ya lugha katika utafiti wa kiswahili: kifani cha mradi wa salamaen_US
dc.typeThesisen_US


Files in this item

Thumbnail

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record