Show simple item record

dc.contributor.authorOtuoma, Damarice A
dc.date.accessioned2015-12-21T09:18:43Z
dc.date.available2015-12-21T09:18:43Z
dc.date.issued2015
dc.identifier.urihttp://hdl.handle.net/11295/93905
dc.description.abstractKatika utafiti huu tunalenga kuchanganua vibonzo katika gazeti la Taifa Leo. Matumizi ya mikakati ya vibonzo katika diskosi huweza kuzua utata katika kufasiri ujumbe ulionuiwa kumfikia msomaji. Tamko la msemaji au mwandishi fulani huweza kufasiriwa na msomaji kwa njia mbalimbali hasa wanapotumia vibonzo kuwasilisha ujumbe wao. Hali kama hii huibua hisia mbalimbali kulingana na ujumbe ulioko pale na hata kutatua mawasiliano. Utafiti huu ulinuiwa kubaini jinsi ambavyo vibonzo vinavyodhihirika katika kuleta dhana ya Ugatuzi kwenye gazeti la Taifa Leo. Vilevile utafiti huu umenuiwa kuonyesha jinsi mikakati hiyo inavyoathiri ufasiri wa ujumbe unaodhamiriwa na mwandishi wa vibonzo; malengo ya utafiti huu ni kuchanganua vibonzo vinavyobeba maudhui ya Ugatuzi, kuchunguza mbinu ya lugha inayopendelewa sana katika kuwasilishavibonzo hivyo na kuchanganua mitindo ya lugha inayotumika katika utunzi wa vibonzo hivyo. Nadharia ya Utambulisho/ Ujihusishaji ya Giles imetuongoza katika utafiti huu. Data kuhusu vibonzo vinavyoleta dhana ya Ugatuzi vimekusanywa kwa njia ya uchanganuzi wa yaliyomo ambapo nakala 50 za magazeti ya Taifa Leo ya mwaka 2010-2014 zilihusishwa . Mikakati mbalimbali ya kipragmatiki kama vile , matumizi ya jazanda, kinaya, chuku, sitiari, yote yaliweza kubainishwa. Aidha utafiti huu umedhihirisha kuwa matumizi ya kinaya na jazanda katika vibonzo juu ya Ugatuzi ndiyo iko katika kiwango cha juu zaidi kwa asilimia 64% na mengine kuchukua yaliyosalia.en_US
dc.language.isoSwahilien_US
dc.publisherUniversity of Nairobien_US
dc.titleMitindo na maudhui katika uchanganuzi wa vibonzo kwenye gazeti la taifa leoen_US
dc.typeThesisen_US


Files in this item

Thumbnail

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record