Fonolojia Arudhi Ya Nomino Mkopo Za Kikeiyo Kutoka Kiswahili
View/ Open
Date
2017Author
Kolongei, Purity C.
Type
ThesisLanguage
enMetadata
Show full item recordAbstract
Utafiti huu una lengo la kuchanganua fonolojia arudhi ya nomino mkopo za Kikeiyo kutoka kiswahili sanifu. Uchanganuzi umetumia nadharia ya fonolojia vipandesauti huru inayochukulia kwamba vipandesauti vinafaa kuwakilishwa katika rusu na kila rusu huwakilisha sifa tofautitofauti. Nadharia hii imetumika kuchanganua miundo ya silabi na toni katika Kikeiyo. Nadharia ya fonolojia mizani nayo imetumika kuchanganua sifa ya mkazo katika Kikeiyo. Fonolojia ya Kikeiyo ilichunguzwa kwa kuangazia mifumo ya vokali na konsonanti ambazo hukutanishwa kuunda silabi. Miundo mbalimbali ya silabi ilielezwa. Toni na silabi ni vipashio ambavyo huwekwa kwenye silabi. Iligunduliwa kuwa uzani wa silabi huathiri mahali mkazo huwekwa katika Kikeiyo. Baada ya kuchanganua fonolojia ya Kikeiyo na kulinganua na ya Kiswahili, ilionekana kwamba nomino zinapoingizwa kutoka Kiswahili hupokea sifa za kiarudhi za Kikeiyo. Miundo ya silabi inabadilika na pamoja na miundo hii, nafasi ya mkazo inasongezwa. Toni hudhihirika katika nomino mkopo tofauti na nomino hizi asilia kwa sababu Kiswahili si lugha toni.
Publisher
University of Nairobi
Rights
Attribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United StatesUsage Rights
http://creativecommons.org/licenses/by-nc-nd/3.0/us/Collections
The following license files are associated with this item: