Sajili Ya Sheria: Mtazamo Wa Vitendo Usemi
Abstract
Utafiti huu unalenga kuchunguza sajili ya sheria kwa mtazamo wa vitendo usemi. Sajili hii itachunguzwa kwa mujibu wa nadharia ya vitendo usemi. Kazi katika tasnifu hii imepangwa katika sura tano, ambapo sura ya kwanza tutaangazia utangulizi kuhusu mada ya utafiti. Sura hii itatuelekeza kuhusu kile kitakachotafitiwa katika kazi hii. Sura ya pili tutachunguza kategoria za vitendo usemi katika sheria. Sura ya tatu itahusu umuhimu wa vitendo usemi kwa wanasheria. Katika sura ya nne tutachunguza mchango wa vitendo usemi kwa sajili ya sheria. Sura ya tano ni muhktasari, mahitimisho na mapendekezo. Data hii itawasilishwa kwa njia ya maelezo, mifano na mijadala katika sura hizi.
Matumiziya vitendo usemi katika diskosi ya sheria yametuwezesha kubaini kuwa, lugha ya sheria ni lugha tendaji kwani kila usemi katika sheria una jukumu tekelezi. Tumebainisha kuwa vitendo usemi hutumiwa na wanasheria ili kufanikisha malengo yao kikazi. Kwa kufanya hivi, kategoria mbali mbali za vitendo usemi hutumiwa na wanasheria. Utafiti huu umebainisha kuwa asilimia kubwa ya vitendo usemi hutumiwa na mawakili ikiliganishwa na mahakimu. Utafiti huu umebaini kuwa vitendo usemi huwa na umuhimu kwa matapo haya mawili ya wanasheria. Yaani, mawakili na mahakimu. Matumizi ya vitendo usemi huwawezesha kufanikisha kazi zao kisheria.
Publisher
University of Nairobi
Rights
Attribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United StatesUsage Rights
http://creativecommons.org/licenses/by-nc-nd/3.0/us/Collections
- Faculty of Arts [606]
The following license files are associated with this item: