Usawiri Wa Ndoa Katika Riwaya Ya Unaitwa Nani?
View/ Open
Date
2013-11Author
Karinge, Joyce W
Type
ThesisLanguage
enMetadata
Show full item recordAbstract
Katika tasnifu hii, tumechunguza usawiri wa asasi ya ndoa katika riwaya ya Unaitwa
Nani? ya K. W. Wamitila (2008). Tunatumia nadharia ya sosholojia ya fasihi kuihakiki
riwaya hii. Tasnifu yetu ina na sura tano.
Katika sura ya kwanza tumeeleza tatizo letu la uchunguzi, madhumuni ya utafiti wetu
pamoja na nadharia tete. Tumeeleza sababu za kuchagua somo hili na misingi ya nadharia
ya sosholojia. Hatimaye, tunachunguza yaliyoandikwa kuhusu somo hili, nadharia ya
sosholojia ya fasihi na muhtasari wa riwaya ya Unaitwa Nani? (2008). Tumeeleza njia
ambazo tumetumia katika utafiti wetu na mwishowe, hitimisho.
Katika sura ya pili tumefiti jinsi asasi ya ndoa imesawiriwa katika riwaya ya Unaitwa
Nani? (2008) kwa kuchanganua ndoa zilizoko katika riwaya husika na kutathmini
mchango wa kila mwanandoa mhusika katika kuiimarisha au kuizorotesha ndoa yake.
Katika sura ya tatu tumezichanganua changamoto zinazoikabili asasi ya ndoa kama
zilivyosawiriwa katika riwaya ya Unaitwa Nani?.
Katika sura ya nne tumechunguza mikakati ambayo jamii ya riwaya ya Unaitwa Nani?
inatumia kuikomboa asasi ya ndoa isisambaratike.
Sura ya tano imekuwa hitimisho la utafiti wetu. Tumetathmini kufaulu au kutofaulu kwa
utafiti wetu kwa kutathmini matokeo ya uchunguzi wetu, ama yanalingana au hayalingani
na madhumuni ya utafiti. Tumeangalia iwapo nadharia tete zetu zimethibitishwa kuwa za
kweli au la. Tumetoa mapendekezo ya utafiti wa baadaye.
Citation
Karinge,Joyce W.;Novemba,2013.Usawiri Wa Ndoa Katika Riwaya Ya Unaitwa Nani?.Publisher
University of Nairobi College of Humanities and Social Sciences