Mofosintaksia ya kishazi cha kitikuu : mtazamo wa uminimalisti
Abstract
Utafiti huu ni jaribio la uchanganuzi wa kiufafanuzi wa kimofosintaksia wa kishazi kikuu cha Kitikuu, lahaja mojawapo ya Kiswahili kwa mtazamo wa nadharia ya uminimalisti. Kishazi kikuu ni aina ya kishazi kinachoweza kujisimamia pekee bila utegemezi, yaani kishazi hum.
Kazi hii imegawika katika sura sita. Sura ya kwanza ni utangulizi wa kazi hii. Tunaanza na kutanguliza juu ya lahaja ya Kitikuu, somo 1a utafiti, madhumuni ya utafiti, nadharia tete, sababu za kuchagua somo, upeo na mipaka, udurusu wa ya1iyoandikwa, msingi wa nadharia ya uminima1isti na mwisho njia za utafiti. Sura ya pili inahusu uainishaji wa nge1i kimofolojia na kisintaksia. Sura ya tatu tumeangazia kirai nomino cha Kitikuu na vipashio vyake. Sura ya nne ni kirai tenzi cha Kitikuu na vipashio vyake, mofo1ojia ya vitenzi na aina ya vitenzi. Sura ya tano tumeshughu1ikia kishazi kikuu cha Kitikuu na vile kanuni ya ukaguzi wa sifa na usogezi unavyofanya kazi. Kwa hiyo matumizi ya nadharia ya uminimalisti inatumiwa katika sura hii. Sura ya sita ni hitimisho na mapendekezo.
Publisher
University of Nairobi, CEES, Kenya
Subject
Swahili language -- SyntaxDescription
(data migrated from the old repository)
Collections
- Faculty of Education (FEd) [5963]