Matumizi Ya Istiari, Tashbiha Na Taashira Katika Diwani Ya Sauti Ya Dhiki
Abstract
Katika tasnifu hii tumeonyesha matumizi ya tamathali tatu za ulinganisho ambazo ni istiari,
tashbiha na taashira katika diwani ya Sauti ya Dhiki iliyoandikwa na Abdilatif Abdalla (1973).
Utafiti umeonyesha kwamba Abdilatif alitumia tamathali hizi tatu kati ya zingine ambazo
hazijashughulikiwa katika utafiti kufikia dhamira yake kwa hadhira yake teule. Ni mashairi
ishirini tu tumeshughulikia ambayo tulichagua kwa kutumia sampuli ya kusudi.
Katika utafiti huu, nadharia ya uhakiki wa mtindo imetumika ambapo baadhi ya vigezo vyake
vimehusika. Nadharia hii iliwezesha kuhakiki viashiria vilivyotumika kuunda tamathali za semi;
istiari, tashbiha na taashira katika diwani ya Sauti ya Dhiki na kuvipa maana viashiria hivi.
Matokeo ya utafiti ni kuwa mwandishi alitumia tamathali za semi; istiari, tashbiha na taashira
kwa njia ya kufana na kufikia dhamira yake ya kuficha ujumbe ili usifikie wasiolengwa, kuleta
tafsida, kujenga mshikamano wa kisemantiki, kufikia umbuji wa mashairi pamoja na kuboresha
kazi yake.Tasnifu hii imeleta uelewa zaidi ya tamathali hizi.
Citation
Master of ArtsPublisher
University of Nairobi