Changamoto za kutafsiri matini za Kisheria: Tathmini ya Katiba ya Kenya (2010)
Abstract
Ikisiri
Kutafsiri matini za kisheria huwa na changamoto nyingi. Changamoto hizi
husababishwa na sifa za kiisimu kama vile leksia, sintaksia, semantiki na
pragmatiki. Kunayo mambo mengine ambayo si ya kiisimu kama vile tofauti za
tamaduni za jamii husika na tofauti za kihistoria ambazo pia huzua changamoto
katika kutafsiri matini za kisheria. Kazi hii imeshughulikia changamoto za
kiisimu za kutafsiri sheria. Hii imefanywa kwa kutathmini sura ya kumi na moja
ya katiba ya Kenya na kutoa mifano mahsusi ya changamoto hizi kama
zinavyojitokeza katika sura hii. Dhana za tafsiri zimeelezewa kwa ujumla. Sifa
za kijumla za matini za kisheria zimefafanuliwa kwa uwazi na maelezo
yakatolewa ya jinsi sifa hizi zinavyoathiri tafsiri za matini za kisheria kutoka
Kiingereza hadi Kiswahili. Vilevile mikakati ya kukabiliana na changamoto hizi
imeelezewa kwa kina.
x
Vifupisho ya maneno
Publisher
University of Nairobi
Description
Thesis