Mchango wa vijana kuleta mabadiliko chanya katika tamthilia teule za Kiswahili
Abstract
Kazi hii inahusu juhudi za vijana kama mawakala wa mabadiliko chanya katika tamthilia nne za Kiswahili. Tamthilia hizi ni Kifo Kisimani naMaua Kwenye Jua la Asubuhi zilizoandikwa na Kithaka wa Mberia . Pango na Seserumbe, zilizoandikwa na K W. Wamitila ,Tumeongozwa na nadharia ya Ki-Foucault iliyoasisiwa na Micheal Foucault. Huyu ni mwananadharia wa Kifaransa aliyeishi baina ya mwaka wa 1926 hadi 1984. Tunaangazia mtazamo wake kuhusu mahusiano ya mamlaka na upinzani unaozuka pale panapokiukwa maadili ya mahusiano yenyewe. Upinzani tunaouchanganua ni ule unaoongozwa na wahusika
vijana katika tamthilia nne tulizoziteua
Katika sura ya kwanza, tumechunguza maswala ya kimsingi yanayodhamiria kujenga msingi wa utafiti wetu kama vile: Sababu za kushughulikia mada, tatizo la utafiti, yaliyoandikwa kuhusu vijana, upeo na mipaka ya utafiti. Tumeongozwa na nadharia tete zifuatazo: kwamba vijana wamefanikiwa kuyaleta mabadiliko na kwamba wanakabiliwa na changamoto mbalimbali katikajitihada zao. Katika sura ya pili tumeijadili dhana ya vijana na kuyachunguza maovu ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Hapo tumewaonyesha vijana wakikabiliana na maovu hayo ili kuleta mabadiliko chanya.
Katika sura ya tatu tumechunguza mafanikio waliyoyapata vijana katika kuzibadilisha jamii zao. Pia tumechunguza changamoto zinazowakabili katika harakati zao za kuleta mabadiliko chanya Katika sura ya nne tumetoa muhtasari wa utafiti rnzima na mapendekezo ya tafiti zaidi zinazoweza kufanywa kuhusiana na mada yetu.
Publisher
University of Nairobi, Kenya