dc.contributor.author | Njuguna, Muiruri | |
dc.date.accessioned | 2016-11-16T07:11:32Z | |
dc.date.available | 2016-11-16T07:11:32Z | |
dc.date.issued | 2016 | |
dc.identifier.uri | http://hdl.handle.net/11295/97383 | |
dc.description.abstract | Kazi yetu imechunguza vipengele vya fani. Tulifafanua dhana ya fani kwa kusema kuwa, fani ni vipengele vya kisanaa katika kazi ya fasihi. Aidha, fani ni jinsi ambavyo msanii hufinyanga kazi yake ili msomaji apate ujumbe wake kwa njia iliyo nzuri. Kazi yetu imetumia nadharia ya umuundo kuchambua vipengele vya fani. Kazi hii imechunguza vipengele vifuatavyo; Msuko, mandhari na wahusika. Tumechunguza namna mandhari mbalimbali yanavyowaathiri wahusika na kubadilisha misimamo yao kuhusu mambo tofauti.Pia tumechunguza namna mwandishi aliyoendeleza maudhui yake kwa kutumia misuko ya aina mbali mbali. Aidha tumechunguza namna wahusika tofauti walivyotumiwa kukuza maudhui ya kazi hii. Kutokana na uchuguzi huu imebainika kuwa maudhui huimarishwa na mwandishi anapotumia vipengele tofauti vya fani kwa ustadi ili kukuza ujumbe wake.
Hii ni kutokana na kweli kwamba mambo ambayo huelezwa kikawaida hutiliwa mkazo na mbinu za kifani zilizoteuliwa na mwandishi na kwa kufanya hivyo ujumi huimarika,kazi hupata mvuto na hatimaye maudhui hueleweka vyema na kwa ukamilifu. | en_US |
dc.language.iso | en | en_US |
dc.publisher | University Of Nairobi | en_US |
dc.rights | Attribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United States | * |
dc.rights.uri | http://creativecommons.org/licenses/by-nc-nd/3.0/us/ | * |
dc.title | Maudhui Yanavyoimarishwa Na Fani Katika Riwaya Ya Nguvu Ya Sala Ya K.w Wamitila | en_US |
dc.type | Thesis | en_US |