Upanuzi Na Ubanaji Wa Maana Katika Kandanda: Ulinganisho Na Ulinganuzi Nchini Kenya Na Tanzania
View/ Open
Date
2023Author
Annah Nyarangi Kibwage, Annah N.
Type
ThesisLanguage
otherMetadata
Show full item recordAbstract
Utafiti huu unahusu upanuzi na ubanaji wa maana katika kadanda nchini Kenya na Tanzania. Tumebainisha kwa kulinganisha na kulinganua namna lugha ya Kiswahili inavyotumika katika utangazaji wa kandanda nchini Kenya na Tanzania, upanuzi na ubanaji wa maana za maneno katika utangazaji wa kandanda katika Kiswahili na kueleza sababu zinazopelekea kuwepo kwa mabadiliko ya kisemantiki katika lugha ya kandanda. Tumeongozwa na Nadharia ya Pragmatiki Leksika katika uchanganuzi wa data yetu. Tulisikiliza matangazo ya moja kwa moja kwenye mtandao wa YouTube na pia kuzisoma taarifa za magazeti kuhusu mchezo wa kandanda. Imetokea kuwa kuna tofauti baina ya lugha ya kandanda inayotumika nchini Kenya na Tanzania kwa misingi ya uchanganyaji ndimi, uhawilishaji wa msimbo, matamshi ya maneno na msamiati unaotumika. Hata hivyo, inapokuja katika matumizi ya mizungu ya lugha hatupati tofauti kubwa baina ya lugha ya kandanda ya Kenya na Tanzania. Pia imedhihirika kuwa upanuzi na ubanaji wa maana hujitokeza kote Kenya na Tanzania na sababu za hali hii ni za kiisimu pamoja na mikakati ambayo imeweza kujibainisha wazi kama vile upolisemia, mazingira, urahisishaji wa mazungumzo, athari za lugha ya kwanza, analojia, utohozi, utiaji wa misamiati mipya, kufupisha maneno na kuambatanisha maneno.
Publisher
University of Nairobi
Rights
Attribution-NonCommercial-NoDerivs 3.0 United StatesUsage Rights
http://creativecommons.org/licenses/by-nc-nd/3.0/us/Collections
- Faculty of Arts [657]
The following license files are associated with this item: