Maudhui ya kiukombozi katika diwani ya jicho la ndani iliyoandikwa na Said A. Mohamed
View/ Open
Date
2015-10Author
Mwazani, Zani E
Type
ThesisLanguage
enMetadata
Show full item recordAbstract
Katika tasnifu hii tumetathmini maudhui ya kiukombozi katika diwani ya Jicho la Ndani, iliyoandikwa na Said A. Mohamed (2002). Utafiti umeonyesha kwamba Said A. Mohamed amezingatia sana maudhui haya ya kiukombozi katika diwani hii. Hata hivyo tuligundua pia kwamba Said A. Mohamed alishughulikia maudhui mengine pia yakiwemo yale ya unyumba, siasa, dini na kadhalika. Tumeyasoma mashairi yote 96, na kugundua kwamba takriban mashairi 62 yameshughulikia mada hii ya ukombozi kwa njia moja au nyingine. Katika utafiti wetu, tumetumia nadharia ya uhalisia wa kijamii, na vigezo vyake vimetumika vilivyo katika utafiti huu. Nadharia hii iliwezesha kuhakiki maudhui ya kiukombozi kufungamana na mfumo wa jamii husika. Matokeo ya utafiti wetu yalidhihirisha kwamba mwandishi aliyashughulikia pakubwa maudhui ya kiukombozi, nia yake ikiwa ni kuwazindua wanyonge waione haja ya kujipigania waupate ukombozi.
Publisher
University of Nairobi
Collections
- Faculty of Education (FEd) [5963]